Skip to main content

Posts

Sura Ya Nne

4. Barabara Iliyopita Msituni. Baada ya masaa kidogo barabara ikaanza kuwa mbovu, na mwendo ukawa mgumu. Kifukuzakunguru akaanza kujikwa na kuanguka juu ya matofali ya manjano, hapa hayakuwa na mpangilio mwema. Wakati mwingine yalikuwa yamevunjika na kuwa hayapo, na kuacha mashimo ambayo Toto aliruka na Dorothy akaizunguka. Lakini kwa sababu Kifukuzakunguru hakuwa na akili alitembea tu na kuanguka chini kwenye matofali magumu. Hakuumia lakini, Dorothy alimwinua na kumsimamisha huku wakimcheka alivyoanguka .
Recent posts

Sura Ya Tatu

3. Jinsi Dorothy Alivyomuokoa Kifukuzakunguru Dorothy alipoachwa peke yake alianza kuhisi njaa. Basi akaenda kabatini akajikatia kipande cha mkate kisha akapaka siagi. Alimpa Toto pia mkate, akachukua ndoo na akaenda mtoni kuteka maji. Toto alikimbia mitini ambapo aliwaona ndege na akaanza kuwabwekea. Dorothy alimfuata na hapo mitini aliweza kuona matunda matamu ambayo alichukua kidogo ili ale kama staftahi. Akarudi tena kwenye nyumba na baada ya kutuliza kiu kwa maji matamu ya mto alianza kupanga safari yake ya kuelekea Jiji la Zumaride. Dorothy alikuwa na rinda moja nyingine tu lakini hilo lilikuwa safi na lilikuwa limeanikwa kwenye msumari kando ya kitanda chake. Nalo hili lilikuwa la madoadoa ya rangi ya samawati na nyeupe. Lakini rangi ya buluu ilikuwa imepungua umaridadi wake baada ya kuoshwa mara nyingi, lakini bado ilikuwa nguo nzuri sana. Msichana alinawa kwa uangalifu na kuivalia nguo hio ya bafia yenye madoafoa.Akavalia kofia yake ya kujikinga kutokana na jua iliyokuwa rangi

SURA YA KWANZA HADI YA TATU.

Utangulizi     Ngano. masimulizi, hekaya na hadithi nyingine zimekuwa za utotoni tangu jadi. Kila mtoto mdogo mwenye afya anazipenda kwa moyo wake wote hadithi hizi kuhusu mambo ya ajabu. Fari zenye bawa, zilizobuniwa nao Grimm na Andersen, zimeleta furaha tele katika mioyo ya watoto kuliko hadithi zote alizobuni mwanadamu.     Lakini hadithi hizi zinazohusu fari, zilizohudumuia vizazi sasa zinaweza kuwekwa katika sehemu ya vitabu vya ‘kihistoria’ katika maktaba ya watoto; wakati umefika kwa hadithi mpya za ajabu nazo zile zilizoeleka za jini,dwafu na fari kuondolewa, pamoja na mambo yote ya kutisha yaliyowekwa na watungaji hadithi ili kutoa funzo. Elimu ya kisasa inawapa watoto maadili; kwa hivyo mtoto wa kisasa anahitaji tu burudani katika hadithi zake. Mtoto huyu anatupilia mbali kwa furaha vitukio vyote asivyokubaliana navyo.     Tukiwa na fikra hizi akilini, hadithi ya “ Mganga Ajabu wa Au” iliandikwa kwa lengo moja tu la kuwafurahisha watoto wa siku hii. Hadithi hii inalenga kuwa

Wasomaji

Kama ungependa kusoma kitabu chote cha Mganga Ajabu Wa Au, nitumie ujumbe nami nitakapomaliza kuitafsiri utakuwa wa kwanza kuipata. Chapisho hili halitakuwa na makosa ya kisarufi kama ilivyosasa.

Mganga Ajabu Wa Au, Sura ya Pili

2. Kongamano la Dorothy na Watu wa Kushangaza. Aliamshwa na kishindo kikubwa dorothy asingalikuwa amelala kitandani angeumia. navyo ilivyokuwa kishindo kilimfanya astaajabu na kufikiri kilichofanyika; naye Toto akiiweka pua yake baradi usoni mwake dorothy na whined dismally. Dorothy aliamka na akangalia kila mahali. Nyumba ilikuwa imewacha kusonga; na pia sasa hapakuwa na giza, kwani jua lilikuwa likiwaka kupitia kioo, kujaza chumba chote. Dorothy alitoka kitandani naye toto akimfuata nyuma akiimbia na akaenda akalifungua mlango. Msichana mdogo aliwika kwa furaha kwa sababu ya mambo yote ya ajabu aliyoyaona macho yake yakipanuka yakawa kubwa kama sahani. Kimbuga kilikuwa kimeitua nyumba kwa utulivu- kwa kimbuga- katika nchi ya urembo tele. Palikuwa na nyasi yenye rangi ya kijani kibichi nayo miti ilikuwa kubwa na iliyokuwa na matunda makubwa yalionekana tamu sana.Kulikuwa na maua chungu nzima kila mahali alipotazama, ndege wenye rangi ambazo ahakuwahi kuona maisha yake yote yen

Mganga Ajabu Wa Au, sura ya kwanza

MGANGA AJABU WA AU 1. Kimbuga Dorothy aliishi katikati mwambuga kubwa huko Kansas na mjombake Henry aliyekuwa mkulima, pamoja naye shangaziye Em aliyekuwa mkewe mkulima. Nyumba yao ilikuwa ndogo,kwa sababu mbao zilizotumiwa kuitengeneza ilibidi zibebwe maili nyingi. Kulikuwa na kuta nne, sakafu na paa, zilizounda chumba kimoja; chumba hiki kilikuwa na jiko iliyokuwa imejaa kutu, kabati palipowekwa sahani, meza, viti vitatu au vinne, na vitanda. Mjomba Henri na shangazi Em walikuwa na jitanda kona moja, naye Dorothy kijitanda kona nyingine. Hapakuwa na $$$$ hata, pia hapakuwa na $$$ isipokuwa shimo ndogo iliyochimbwa ardhini, iliyoitwa $$$ ya kimbuga, mahali ambapo familia ingekimbia kama mojawapo wa upepo mkubwa ungezuka , iliyokuako kubwa kubwa kiasi cha kuvunja na kuharibu nyumba yoyote pahali popote ilipopita. Ili uingie $$$ ya limbuga ulifungua mlango mdogo katikati mwa sakafu, ambapo palikuwa na ngazi iliyoshuka mpaka ndani mwa shimo hii ndogo iliyokuwa na giza. Dorothy ali